
Katika msimu huu wa kilimo wa 2022/2023 wakulima wa zao la alizeti watanufaika kwa kupata mbegu hizo za ruzuku, ikiwa ni mkakati wa serikali katika kukuza Zaidi zao hilo la alizeti, Dkt. Sophia Kashenge mtendaji mkuu wa wakala wa mbegu nchini ASA hapa anabainisha mkakati wa serikali katika kufikia malengo
Kupitia mbegu hizo halmashauri ya Itigi mkoani Singida imepokea shehena ya mbegu hizo zitakazosambazwa kwa wakulima kama anavyosema afisa kilimo, mifugo na uvuvi wa halmashauri hiyo
Kwa upande wao wakulima wameonesha kuwa na Imani katika mpango huo wa mbegu za rukuzu katika kukabiliana na tatizo la uhaba wa Mafuta ya kula.