Jumanne , 14th Apr , 2020

Stori kubwa iliyokuwepo siku ya leo Aprili 14, 2020, katika habari za burudani ni juu ya kujitoa kwa wasanii Killy na Cheed katika lebo ya Kings Music Records, ambayo inasimamiwa na msanii Alikiba.

Mkali wa BongoFleva Alikiba

Sasa muda mfupi uliopita Alikiba ameweka maelezo katika mtandao wa Instagram, ambayo inatafsirika kama fumbo flani hivi baada ya wasanii wake kujitoa katika lebo ambayo yeye anaisimamia.

Katika post hiyo Alikiba ameweka picha ya mkongwe wa BongoFleva Dully Sykes kisha ameandika "Unapomtendea mtu jambo lake tena kwa mapenzi yote usitarajie fadhila wala malipo baadae kwa sababu kuna aina nyingi ya binadamu, sio kila mmoja ana moyo kama wako".