Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo
Mrisho Gambo ametoa kauli hiyo wakati alipofanya ziara ya kutembelea Hospitali ya Wilaya ya Arusha, ambayo inasubiliwa na wananchi kwa muda mrefu.
"Uboreshaji wa miundombinu ya Afya, ikiwemo ujenzi na ukarabati wa vituo vya Afya, Zahanati pamoja na Hospitali ya Wilaya ya Arusha, utapunguza adha ya kutembea umbali mrefu kwa wananchi na baada ya hapo tutawahamisha wananchi waanze kutumia bima" amesema RC Gambo.

