
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangalla.
Akijibu swali bungeni mjini Dodoma hii leo Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangalla amekiri kuwa tatizo la vifo vya wajawazito na watoto ni kubwa nchini hususan katika maeneo ya vijijini kutokana na kukosa huduma za upasuaji wa dharura na wakupanga.
Dkt. Kigwangalla amesema pamoja na hayo serikali inaendelea kutekeleza mpango mkakati wa kuvijengea uwezo vituo vya afya hasa vilivyopo vijijini ili viweze kutoa huduma ya upasuaji hasa wa dharura.
Aidha, Naibu Waziri huyo ameongeza kuwa serikali ikishirikiana na wadau mbalimbali inaendelea kuboresha miundombinu, watumishi, upatikanaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi ili kuokoa maisha ya akina mama wengi walio vijijini.