
Mbunge wa jimbo la Kyela mkoani Mbeya, Dkt Harrison Mwakyembe
Kutokana na athari hizo kwa wakazi wa Wilaya hiyo uongozi wa Wilaya hiyo ukiongozwa na Mbunge wa Kyela Dkt. Harrison Mwakyembe ameomba msaada kutoka katika makampuni mbalimbali nchini kutoa misaada ya kuwasaidia waathirika wa mafuriko katika Wilaya hiyo.
Dkt.Mwakyembe amesema wakazi hao wameathirika kwa kiasi kikubwa ambapo kwa sasa wanahitaji msaada wa Chakula,Mavazi na sehemu ya kujihifadhi wakati wakianza utaratibu wa kukarabati Nyumba zao.