Katika taarifa yake Kocha wa Stars Charles Boniface Mkwasa amesema, wachezaji wote wapo salama isipokuwa mchezaji mmoja Abdi Banda ambaye ni majeruhi na hatokuwepo katika mechi hiyo, huku akiamini juhudi, ushirikiano na uelewa wa wachezaji ndio njia ya ushindi katika mechi hiyo.
Kwa upande wa wapinzani wao kikosi cha timu ya Nigeria Super Eagles kinatarajia kuwasili nchini siku yoyote kuanzia hii leo kwa ajili ya maandalizi ya mechi hiyo.

