(Alexander Zverev akiondoka uwanjani)
Zverev raia wa Ujerumani amefukuzwa kwenye michuano hiyo ya wazi ya Mexico kwa kitendo cha kugonga kiti na miguu ya mwamuzi huyo akiwa anarudi kukaa kwenye kiti chake baada ya mchezo kumalizika na kupigiza raket yake mara tatu kwa nguvu na hasira katika miguu ya mwamuzi anayekaa juu katikati ya uwanja usawa wa wavu baada ya kufungwa seti mbili kwa alama 6 - 2, 4 - 6, na 10 - 6 dhidi ya Lloyd Glasspool.





