
Mchezaji mpya wa Yanga, Gadiel Michael
Wakati huo huo uongozi wa Azam FC kupitia msemaji wa timu hiyo Jaffar Iddi Maganga wamewashukuru viongozi wa Yanga kwa kuwa waungwana na kufika kwenye ofisi zao wakiongozwa na mwenyekiti wa usajili, Hussein Nyika.
"Tumewapunguzia bei imekuwa nusu yake na taratibu zote zimekamilika baada ya pande zote kukubaliana ni rasmi sasa, tunathibitisha ni ruksa kwa Yanga kumsajili Gadiel kwa msimu ujao na tunamtakia kila la kheri katika maisha yake mapya ndani ya timu hiyo", amesema Maganga.
Msemaji wa timu ya Azam Fc, Bwana. Jaffar Iddi Maganga
Kwa upande mwingine, Maganga amesema siyo jambo la kweli kuwa wachezaji wakitaka kuenda klabu ya Simba huwa wanaenda bure ila kwa yanga wanabaniwa kama baadhi ya watu wanavyoeneza uvumi huo.