Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Vita ya Sadick na Mopele kunogesha fainali

Jumamosi , 18th Aug , 2018

Fainali ya michuano ya Kikapu ya Sprite Bball Kings mwaka 2018, inaanza rasmi leo kwa game 1 kwenye 'best of five' kupigwa kwenye uwanja wa taifa wa ndani ikikutanisha mabingwa watetezi Mchenga Bball Stars dhidi ya Flying Dribblers.

Kushoto ni Baraka Sadick wa Mchenga Bball Stars na kulia ni Baraka Mopele wa Flying Dribblers.

Kuna vitu mbalimbali vya kuvutia kwenye fainali hizo ambapo vita ya pointi inaonekana kuwa kivutio namba moja ikiwa hadi sasa mchezaji Baraka Sadick wa Mchenga Bball Stars anaongoza kwa kufunga pointi nyingi katika tyimu hizi mbili zilizoingia fainali akiwa na jumla ya pointi 100.

Anaye mfuatia kwa karibu ni Baraka Mopele kutoka timu ya Flying Dribblers ambaye mpaka sasa kafunga pointi 92, hivyo wawili hawa watakuwa wanaziongoza timu zao kuelekea kuzipata zile milioni 10 kwa bingwa, milioni 3 kwa mshindi wa pili na kubwa zaidi kwao kama wachezaji ni ile zawadi ya mchezaji bora yaani 'MVP' ambayo ni milioni 2.

Mbali na hilo timu zote zimefanya mabadaliko ya wachezaji ambao walishiriki msimu uliopita, wengine wakiwepo na wengine hawapo. Kwa upande wa Mchenga Bball Stars wao wameongeza sura mpya lakini wengi wamebaki walewale ila wanamkosa Rwehabura Munyagi ambaye ndio alikuwa MVP wa mashindano mwaka 2017. 

Kikosi chao cha msimu  huu kina nyota kama Baraka sadick, Cristian Joseph, Jije Makani, Mgosi Nyameta, Johnson Mohamed, Mohamed Yusuf, Cornelius Mgaza, Ivan Tarimo, Amos Christian na Masero Nyirabu.

Kwa upande wa Flying wao pia wamefanya mabadiliko lakini kikosi chao kimebaki na asilimia kubwa ya wachezaji waliokuwepo msimu uliopita. Mchezaji ambaye wanamkosa uwanjani ni Geofrey Lea lakini wapo naye kwa upande mwingine akiwa kama kocha msaidizi.

Kikosi chao kamili kina wachezaji kama Habirmana Mayeye, Baraka Mopele, Shenta Denis, Elias Samwel, Benedict Kafuru, Mussa Hassan, Steve Mtemihonda, Meddy Makani, Hermes Lazaro na John Mashauri.
 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa