Kipigo hicho cha Nigeria Inayofundishwa Christopher Musa Danjuma kinakuwa cha pili kwa Tanzania, baada ya awali kufungwa 1-0 na Ivory Coast katika mchezo wa kwanza hivyo kuishia hatua ya makundi.
Super Falcons sasa inajihakikishia kwenda Nusu Fainali za michuano hiyo kwa pointi zake sita baada ya kuwafunga wenyeji Kongo 5-1 katika mchezo wa kwanza.
Mchezo mwingine wa kundi hilo uliwakutanisha Kongo na Ivory Coast ambapo Ivory Coast iliwachapa wenyeji bao 1-0.
Nigeria itamaliza na Ivory Coast, wakati Tanzania na Kongo wakimalizia michezo yao ya mwisho ya makundi huku wakiwa wamepoteza michezo miwili.
Kikosi cha Nigeria kilikuwa; Oluehi Tochukwu, Edoho Blessing, Osinachi Marvis Ohale, Osarenoma Igbinovia, Onome Ebi, Gladys Akpa, Wogu Chioma Success, Ugochi Desire Oparanozie, Ukpong Esther Sunday, Adeboyejo Yetunde Oluwatosin na Nwabuoku Evelyn Chiedu.
Tanzania; Fatuma Omar Jawadu, Anastas Katunzi, Stumai Athumani, Amina Bilal, Fatuma Issa Maonyo, Donisia Minja, Mwanahamisi Shurua, Happyness Hezron, Fatuma Salum, Asha Rashid na Sophia Mwasikili.

