
Matukio ya kimichezo mwaka 2019
Kenye tasnia ya masumbwi mwaka 2019 umekuwa mzuri, yakifanyika marekebisho ya sheria za vyama vinavyoongoza mchezo huo pamoja na kuendelea kukua kwa mabondia wengi nchini. Mfano mkubwa ni Hassan Mwakinyo ambaye amecheza mapambano mawili makubwa, likiwemo lile alilocheza dhidi ya Arnel Tinampay wa Ufilipino.
Zifuatazo ni baadhi ya tweets zinazoonesha matukio makubwa yaliotokea katika michezo kwa mwaka 2019.
Mwaka 2019 umeshuhudia kukua kwa tasnia ya masumbwi hasa baada ya kufanyika pambano kubwa kati ya Hassan Mwakinyo na Mfilipino Arnel Tinampay katika uwanja wa Uhuru na kufuatiliwa kwa kiasi kikubwa.
Mwakinyo alishinda pambano hilo kwa pointi.#FungaMwakaSpecial pic.twitter.com/TKAe811uyY
— East Africa TV (@eastafricatv) December 31, 2019
Michuano ya Sprite Bball Kings ilifanyika kwa mara ya tatu mfululizo mwaka 2019, Mchenga Bball Stars wakifanikiwa kushinda ubingwa bila kupoteza mchezo wowote, wakiifunga Tamaduni na mchezaji Baraka Sadick (Mchenga) akiibuka MVP.#FungaMwakaSpecial pic.twitter.com/NdjZTNFWbj
— East Africa TV (@eastafricatv) December 31, 2019
Moja ya matukio makubwa yaliyotikisa kwenye soka mwaka 2019 ni kufutwa kazi kwa kocha wa @SimbaSCTanzania Patrick Aussems kutokana na utovu wa nidhamu na kutofikia malengo, pia mahasimu wao @yangasc1935 wakimfuta kazi kocha Mwinyi Zahera.#FungaMwakaSpecial pic.twitter.com/VykQx400dW
— East Africa TV (@eastafricatv) December 31, 2019
Tukio lingine ambalo halitosahaulika ni rekodi ya nahodha wa Taifa Stars na klabu ya Genk, Mbwana Samatta ambaye katika mwaka 2019 akiwa na klabu yake ya Genk ameweka rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kucheza michuano ya Klabu Bingwa Ulaya na kufunga bao, akifunga jumla ya mabao matatu katika hatua ya makundi ikiwemo Liverpool.
Mwaka 2019 tumeendelea kushuhudia kuongezeka kwa idadi ya nyota wa Tanzania wanaocheza Kimataifa na kuona mafanikio yao, wakiwemo @Samagoal77_ Simon Msuva, Himid Mao, Kelvin John, Abdi Banda, Shiza Kichuya.#FungaMwakaSpecial pic.twitter.com/yc0y09kEHP
— East Africa TV (@eastafricatv) December 31, 2019