Jumanne , 17th Nov , 2015

Timu ya Tanzania Prisons imeanza kujipanga upya ili iweze kufanya vizuri katika mfululizo wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara.

Katibu mkuu wa klabu hiyo Osward Morris amesema, wanaanza mazoezi leo kwa ajili ya maandalizi ya muendelezo wa ligi hiyo.

Morris amesema, wamerudi kujipanga upya ili waweze kufikia malengo yao katika kuhakikisha wanacheza soka la ushindani.

Morris amesema, uongozi wa klabu hiyo unatarajia kukutana leo kwa lengo la kujadili ripoti iliyowasilishwa na kocha wao Salum Mayanga.