(Tembo Warrirors walipokuwa wanacheza na Cameroon kwenye CANAF)
Magoli mawili ya Tanzania yamefungwa na Alfan Kyanga dakika ya 2 na 15 , Ramadhan Chomole dakika ya 18, na Frank Ngailo dakika ya 36 na 44.
Shangwe na nderemo zilianza pindi tu mchezo huo ulipomalizika kwenye dimba la Mkapa Jijini Dar es Salaam kwa kujua pia kutinga nusu fainali huko kinafanya timu nne hizo kukata tiketi ya kucheza kombe la Dunia nchini Uturuki 2022.
Tembo Warriors wamefuzu hatua hiyo mbele ya Waziri mwenye dhamana ya michezo, Mhe. Innocent Bashungwa ambaye alikuwa anawaongoza watanzania luishangilia Tembo Warriors ili kuwapa hamasa ya kufanya vizuri zaidi.
Waziri Bashungwa amesem kwa kuhakikisha kwamba Serikali itaendelea kuiisaidia timu hiyo ili iendelee kufanya vizuri kuelekea hatua zinazofuata ikiwemo maandalizi ya Kombe la Dunia.
Dkt Abbasi Nnae amesema, kwa kuwa safari ya kuelekea kombe la dunia imekamilika kazi iliyobaki ni kuhakikisha kuwa kombe la CANAF linabaki Tanzania.
Kufuzu huko ni pongezi pia kwa kamati maalum ya kitaifa chini ya katibu Mkuu wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassani Abbasi ambayo iliisimamia Tembo Warriorsbila kusahau hamasa ya Rais wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu.
Tembo Warriors ilifungwa 1-0 na Uganda, ikapata ushindi wa 2-1 dhidi ya Morocco, Sierraa Leone 1-0 katika hatua ya makundi na hatimaye kuifunga Cameroon 5-0 kwenye hatua ya nusu fainali ya michuano ya CANAF.
Mchezo huo pia umeshuhudiwa na Rais wa Mashindano hayo duniani, Mateus Wildack.