Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tanzania yatwaa kombe la Kanda ya tatu Afrika

Jumanne , 22nd Nov , 2022

Timu ya Taifa ya Tanzania ya mchezo wa kuogolea (Tanzanite) imeshinda taji la kanda ya tatu Afrika baada ya kuzishinda nchi nyingine tisa zilizoshiriki katika mashindano hayo.

Tanzanite ilikusanya jumla ya pointi 3,061 katika mashindano hayo yaliyofanyika kwenye bwawa la kuogelea la klabu ya Gymkhana.

Ushindi huo ni wa tatu katika historia ya Tanzanite katika mashindano hayo kwani mwaka 2016, Tanzania ilishinda taji hilo mjini Kigali, Rwanda na mwaka 2017 ililitwaa tena katika mashindano yaliyofanyika hapa nchini.

Tanzania iliwakilishwa na wachezaji 63 katika mashindano hayo yaliyodhaminiwa na kampuni ya uzalishaji wa sukari Kilombero Sugar Company kupitia chapa ya Bwana Sukari.

Kwa mujibu wa matokeo ya michuano hiyo, nafasi ya pili ilikwenda kwa waogeleaji walioiwakilisha shirikisho lililosimamishwa la Kenya ambao waliruhisiwa kufanya bila kutumia jina la nchi yao na kujulikana kwa jina la ‘ Swimmers from Suspended Federation. Waogeleaji hao walikusanya pointi 2,768 ambapo nafasi ya tatu ilikwenda kwa Uganda iliyopata pointi 2,521.50.

Zambia ilimaliza katika nafasi ya nne kwa kukusanya pointi 1,878 huku Afrika Kusini ikimaliza katika nafasi ya tano kwa kukusanya pointi 1,385. 50.

Mashindano hayo yalianza tarehe 16 na kumalizika 19 Novemba, 2022 jijini Dar es salaam.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa