Jumatano , 13th Jul , 2016

Klabu ya Stand United ya Mjini Shinyanga inatarajia kumtangaza kocha mpya atakayerithi nafasi ya Mfaransa, Patrick Liewig ambaye mkataba wake umesitishwa mara baada ya kumalizika kwa msimu uliopita wa ligi kuu Tanzania Bara.

kikosi cha Stand United

Mkurugenzi wa benchi la ufundi wa Stand United, Muhibu Kanu amesema kamati ya utendaji ya Stand United ipo katika mchakato wa kumpata kocha mpya ambapo mpaka sasa wamepokea CV za makocha wawili kutoka nje ya nchi na makocha wawili kutoka hapa nyumbani.

Kanu amesema, kufikia siku ya Ijumaa watatangaza jina la kocha mpya na wanategemea kuanza mazoezi na maandalizi ya msimu mpya siku ya Jumatatu ya wiki ijayo.