Hamis Kiiza
Tangu kumalizika kwa Ligi Kuu Bara 2015/2016, kumekuwa na taarifa mbalimbali juu ya kutemwa kwa mshambuliaji huyo kutokana na sababu za utovu wa nidhamu lakini hakukuwa na kiongozi aliyewahi kuthibitisha kuhusiana na hilo zaidi ya kutoa kauli zenye viashiria vya hali kama hiyo.
Aidha, ilielezwa kuwa Kiiza anaweza kutemwa pamoja na Mganda mwenzie, Juuko Murshid kutokana na kufuata mkumbo wa kugoma kuichezea timu hiyo mpaka wapewe mishahara yao.
Kiiza aliyewahi kuichezea klabu ya Yanga anaungana na wachezaji wengine wa kigeni waliotemwa msimu huu ambapo ni Mkenya, Raphael Kiongera, Mrundi, Emiry Nimubona na Mganda, Brian Majwega.



