Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Simba na Yanga watambiana matawini

Jumanne , 21st Feb , 2017

Kuelekea katika mpambano wa watani wa jadi Simba na Yanga, viongozi wa matawi mbalimbali ya vilabu hivyo wameendelea kutambiana huku wakiitaka serikali kumchukulia hatua mtu yeyote atakayegundulika kufanya uharibifu katika mchezo huo.

Mashabiki wa Simba na Yanga Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam

Mwenyekiti wa tawi la Mpira Pesa kwa upande wa Simba Ostadh Masoud amesema, mechi zote wanazokutana na Yanga wanaziheshimu na kikosi cha Simba kimejipanga vizuri na kwa umakini ili kuweza kuibuka na ushindi kwani lengo lao hasa ni ubingwa ili kuweza kuiwakilisha nchi katika mashindano ya kimataifa.

"Lazima tuongeze umakini kwasababu Yanga tulimkimbia kwa pointi nane leo hii ametukuta tunatofautiana kati ya pointi moja au mbili kwa hiyo anaonekana kuna kitu anakitaka kwa maana hiyo lazima niwaambie wana Simba hata wachezaji kwa ujumla hii ni fainali na kila mtu ambaye anaamini ana kitu ambacho kitasaidia Simba ishinde kitumike, " amesema.

Kuhusu vurugu, Ostadh amesema "Mimi niwaambie tuu mashabiki kuwa watulivu katika mchezo wa Februari 25, Mwamuzi akishapuliza kipyenga hakuna wa kupinga hata ukienda mahakama kuu, sisi tujikite kuhakikisha timu yetu inashinda na tusitegee kushindwa au sare, " amesema.

Kwaupande wake Katibu wa tawi Yanga la Tandale kwa Mtogole Waziri Jitu amesema, wanaamini wataibuka na ushindi katika mchezo huo kwani kikosi chake ni bora na Simba wasitegemee kama wataweza kubeba pointi tatu katika mchezo huo.

"Sisi tunajiamini na kazi tumeshamaliza tusubiri tuu siku ya jumamosi tufike Uwanjani kuhitimisha, mimi nina timu bora kwani Afrika Mashariki hii ikiangalia timu bora ya kwanza Yanga na inafuatiwa na Azam FC kidogo, " amesema.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu