Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Simba na Yanga hakuna mafanikio - Uhuru Seleman

Jumatatu , 20th Feb , 2017

Mchezaji wa Kimataifa wa Tanzania anayechezea timu ya Royal Eagles ya nchini Afrika kusini Uhuru Seleman amefunguka na kusema mafanikio yake yamekuja baada ya yeye kutoka katika vilabu vya Tanzania na kwenda nje. 

Uhuru Seleman

 

Uhuru amesema licha ya kuchelewa kutoka katika soka la nyumbani lakini angalau yeye amepata mafanikio ambayo anajivunia kwa sasa, kama vile kuweza kumiliki nyumba zake mwenyewe binafsi, kumiliki biashara mbalimbali na kuweza kuhudumia familia yake. 

"Naweza sema mimi nimechelewa sana kutoka katika soka la nyumbani, lakini hata hivyo bado najivunia vitu kadhaa ikiwemo kuwa na makazi binafsi zaidi ya nyumba moja,  kumiliki biashara na kuhudumia familia bila kuteteleka kwa lolote lakini nikukumbushe tu kuwa kucheza Simba na Yanga siyo wote wanaopata mafanikio unayoyafikiria, mimi vitu vingi nimetimiza baada ya kutoka nje" alisema Uhuru Seleman

Mbali na hilo Uhuru Seleman amezungumzia mchezo ambao utafanyika siku ya tarehe 25 kati ya watani wa jadi Simba na Yanga.

"Kiukweli sijaziangalia timu zilivyo kwa muda mrefu sasa lakini huwa mechi ya Simba na Yanga ni ngumu kuitabiri ukiwa nje ya uwanja" alisema Uhuru Seleman 

Uhuru Seleman anasema kwa sasa yeye hachezi mpira kama mapenzi bali anacheza mpira kama kazi hivyo anaangalia maslahi na kama Simba watamuhitaji tena kuja kucheza katika klabu hiyo hana tatizo ataangalia tu maslahi yake na si kitu kingine.

"Mpira kwangu ni kazi na sichezi mpira kwa mapenzi, ikitokea Simba wananihitaji nitakwenda kukiwa na maslahi katika hilo" alisisitiza Uhuru Seleman 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa