
Kikosi cha Simba SC
Simba imefuzu hatua ya robo fainali baada ya kumaliza nafasi ya pili kwenye kundi D wakiwa na alama 10 sawa na vinara wa kundi hilo RS Berkane. Simba ilifikisha alama hizo baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya us Gendermerie kwenye mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi.
Katika droo ya kesho ya kupanga michezo ya hatua ya robo fainali itakayofanyika makao makuu ya shirikisho la soka barani Afrika CAF huku Cairo nchini misri, Simba inaweza kupangwa na kinara wa kundi A,B au C. timu hizo ni Al-Ahli Sports Club ya Libya, TP Mazembe ya DRCongo na Orlando Pirates ya Afrika Kusini.
Katika hatua hii timu zilizokuwa kundi moja haziwezi kukutana lakini zile zinazotoka kwenye nchi moja zinaweza kupangwa kucheza kwenye hatua hii.