Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Simba Bingwa mpya kombe la Mapinduzi 2022

Ijumaa , 14th Jan , 2022

Wekundu wa Msimbazi Simba wameibuka kuwa mabingwa wa Michuano ya kombe la Mapinduzi mwaka 2022 baada ya usiku wa jana Januari 13, 2022 kuifunga Azam 1-0 kwenye dimba la Amani, Visiwani Zanzibar.

(Wachezaji wa SImba wakisheherekea Ubingwa wa Mapinduzi mwaka 2022)

Bao la pekee la ushindi la SimbaSC limefungwa na mshambuliaji wake, Meddie Kagere dakika 56 kwa mkwaju wa penalty baada ya mlinda mlango wa Azam FC, Mathias Kigonya kumkanya Pape Ousmane Sakho ndani ya eneo la 18.

Ubingwa huo umewafanya Simba kubeba kombe hilo mara ya nne, kufuta uteja mbele ya Azam FC wa kupoteza fainali mbili mbele ya Wanalamba lamba hao pamoja na kujiuliza vema walipopoteza 2021 mbele ya watani wao, Yanga.

Kamati ya mashindano ya Mapinduzi iliwapa zawadi Simba ya Shilingi milioni 25 taslimu kwa kuwa bingwa huku Makamu Bingwa, klabu ya Azam walipewa kiasi cha shilingi milioni kumi na tano taslimu.

Mbali na zawadi za Jumla, lakini kamati hiyo iliendelea kutoa tuzo binafsi kwa wachezaji waliofanya vema ambapo, tuzo ya mfungaji bora imeenda kwa Meddie Kagere, Kipa bora, Aishi Manula na Mchezaji bora Pape Sakho wote wa Simba SC.

Henock Inonga Baka alichaguliwa kuwa nyota wa mchezo wa fainali hiyo baada ya kuonesha umahiri mkubwa wa kuzuia mashambulizi ya Azam FC kwa washambuliaji Rodgers Kola na Idris Mbombo.

Tuzo ya mchezaji bora chipukizi imeenda kwa winga Tepsi Evans, kiungo bora imeenda kwa Kenneth Muguna, beki bora Daniel Amoah wote kutoka kikosi cha mabingwa wa Kihistoria wa michuano hiyo, Klabu ya Azam.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu