Alhamisi , 4th Aug , 2016

Nahodha wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta leo atakuwa dimbani kuendelea na michuano ya kufuzu kushiriki ya Europa League wakati timu yake, KRC Genk itakapomenyana na wenyeji Cork City FC katika mchezo wa marudiano Raundi ya Tatu ya mchujo.

Mbwana Ally Samatta (katikati) akishangilia goli pamoja na wachezaji wenzake wa KRC Genk.

Genk inahitaji kulazimisha sare kwenye Uwanja wa Turner's Cross, mjini Cork, Ireland baada ya awali kushinda 1-0 Alhamisi iliyopita nyumbani.

Pamoja na ugumu uliopo mbele yao, Samatta amesema wanakwenda kutafuta mabao na kujilinda zaidi.

"Tutapambana, maana kwenye mchezo wa marudiano tunatakiwa kwenda kutafuta mabao na kujilinda, tutajitahidi"

Timu zitakazoshinda zitakwenda hatua ya mwisho ya mchujo kuwania kupangwa kwenye makundi, ambako vigogo kama Manchester United ya England wataanzia huko.