Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Sababu za Prince Dube kupelekwa Afrika kusini

Alhamisi , 26th Nov , 2020

Klabu ya Azam FC imethibitisha kuwa mshambuliaji wake Prince Dube amevunjika mkono, mshambuliaji huyo aliumia dakika ya 15 kwenye mchezo wa ligi kuu bara dhidi ya Yanga, na anatarajiwa kwenda Afrika Kusini kwa matibabu zaidi.

Prince Dube ametoa mchango wa mabao 10 ndani ya Azam FC msimu huu kwenye VPL, amefunga mabao 6 na ametoa pasi za usaidizi wa magoli 4

Dube raia wa Zimbabwe ambaye ndio kinara wa ufungaji wa klabu ya Azam msimu huu akiwa na mabao 6, alipata majeraha hayo baada ya kudondoka vibaya alipokuwa anawania mpira wa juu dhidi ya beki wa Yanga Bakari Nondo Mwamnyeto.

Taarifa iliyotolewa na klabu ya Azam inasema mshambuliaji huyo amevunjika mfupa wa mbele wa mkono wake wa kushoto unaoitwa Ulnar, huu ni mfupa unaoanzia kwenye kiwiko na kushuka hadi kwenye kidole cha mwisho.

Pia taarifa hiyo imeweka wazi kuwa Dube Ataondoka nchini Siku ya Jumapili ya Novemba 29, 2020 kuelekea nchini Afrika Kusini kwa matibabu zaidi, katika Hospitali ya Vincent Pallotti iliyopo Cape Town, chini ya daktari bingwa wa mifupa Robert Nicolas.

Azam FC wamekuwa wakiitumia hospital hii kuwatibia wachezaji wao tangu mwaka 2011.

Na kipigo walichokipata Azam FC hapo jana kinakuwa ni cha 3 msimu huu, na sasa wameshuka mpaka nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi wakisalia na alama zao 25 ikiwa ni tofauti ya alama 3 dhidi ya vinara Yanga SC wenye alama 28.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa