
Nyota wa Ureno Cristiano Ronaldo aliyenyoosha kidole akiwa na nyota wa England, Harry Kane.
kuelekea mechi hiyo, Ronaldo anapewa nafasi kubwa ya kuonesha ubabe wake wa kutikisa nyavu baada ya kutikisa kamba za wapinzani mara nne katika mechi mbili alizocheza.
Endapo Ronaldo atafunga bao moja dhidi ya Iran atakuwa amemzidi nyota wa England, Harry Kane aliyefikisha mabao matano katika mashindano hayo.
Mechi nyingine zitakazopigwa ni Misri ambao wameshaaga mashindano watakamilisha ratiba dhidi ya Saudi Arabia majira ya saa 11 jioni huku pia Uruguay wakikipiga na wenyeji Urusi muda huohuo wa saa 11.