Alhamisi , 30th Nov , 2023

Rais wa Yanga Eng. Hersi Said amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa kwanza wa Shirikisho la Klabu za Afrika (ACA) lenye makao yake makuu yake Nairobi Kenya.

Injinia Hersi atasaidiwa na Jessica Motaung wa Kaizer Chiefs kama makamu Mwenyekiti huku Paul Basset wa Akwa United ya Nigeria akichaguliwa kuwa makamu Mwenyekiti wa pili.

Uzinduzi huo uliofanyika Nchini Misri umesimamiwa na Rais wa CAF, Patrice Motsepe nchini Misri huku Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa Simba SC, Salim Try Again akiwa miongoni mwa waliohudhuria.