Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Nyota wa Yanga atua Azam FC, wakijipanga kumtibu

Jumamosi , 26th Mei , 2018

Baada ya sintofahamu ya muda mrefu juu ya hatima ya mchezaji wa kimataifa wa Yanga Donald Ngoma ndani ya klabu hiyo, hatimaye nyota huyo raia wa Zimbabwe amesajiliwa na klabu ya Azam FC.

Taarifa ya Azam FC imesema imeingia makubaliano na mshambuliaji huyo kwaajili ya msimu ujao wa 2018/19. Pamoja na kuthibitisha usajili huo, lakini uongozi wa wanalambalamba umegoma kuweka wazi mkataba baina ya pande
hizo mbili.

Msemaji wa Azam FC Jaffar Idd Maganga, ameenda mbali zaidi kwa kusema tayari mchezaji huyo ameandaliwa jezi namba 11 iliyokuwa ikitumiwa na mshambuliaji Yahaya Mohammed, aliyerejea Aduana Stars ya nchini kwao Ghana, baada ya kufikia makubaliano ya kuvunja mkataba na Azam.

Jaffar amesema baada ya makubaliano hayo na Ngoma, wanatarajia kumpeleka katika Hospitali ya Vincent Pallotti jijini Cape Town, Afrika Kusini kwa ajili ya kumfanyia vipimo vya afya ili kuona ni kwa kiasi gani majeraha yaliyokuwa yakimsumbua yamepona au kama anahitaji matibabu zaidi.

Ngoma alijiunga na Yanga msimu wa 2016/17 akitokea FC Platinum ya Zimbabwe, na alitoa mchango mkubwa kwa Yanga msimu huo, ikifika hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika pamoja na kubeba mataji mawili, Ligi Kuu na Kombe la FA.

Msimu huu unaomalizika Jumatatu ya Mei 28, Ngoma hajawa sehemu ya kikosi cha Yanga, kutokana na kuwa majeruhi kwa muda mrefu ambapo ilifika muda uongozi ukataka kumuondoa. Awali, Ngoma alikuwa na mkataba wa miaka miwili kabla ya mwaka jana kuripotiwa kuongeza tena miwili.
 

HABARI ZAIDI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa