Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ni fainali ya kufa na kupona Zanzibar

Ijumaa , 13th Jan , 2017

Michuano ya Kombe la Mapinduzi inahitimishwa leo visiwani Zanzibar kwa mchezo wa fainali ya kufa na kupona kati ya matajiri wa Dar es Salaam timu ya Azam FC dhidi ya mabingwa wa kihistoria wa kombe hilo, wekundu wa Msimbazi, Simba SC.

Mchezo huo wa fainali unapigwa majira ya saa 2:15 usiku, ambapo timu zote zinaingia dimbani zikiwa na takwimu zinazokaribia kulingana, ambapo Simba imefungwa goli moja pekee huku Azam ikiwa haijafungwa goli hata moja.

Simba imeingia fainali baada ya kuifunga Yanga kwa penati 4-2 katika hatua ya nusu fainali wakati Azam ikiwa imeifunga Taifa Jang'ombe bao 1-0.

Simba inatafuta rekodi ya kuendelea kuwa na makombe mengi katika michuano hii kwa hadi sasa imekwisha beba ndoo hizo mara 3 wakati Azam ikibeba mara mbili pekee.

Afisa habari wa Azam FC Jaffar Iddi Maganga 'Mbunifu' amesisitiza kuwa kikosi chao kipo imara na kipo tayari kwa ajili ya kuikabili Simba ambayo imeonekana kuimarika kwa msimu huu.

Kwa upande wa wekundu wa msimbazi Simba Makamu wa Rais wa klabu hiyo Geofrey Nyange Kaburu amesema watashusha kikosi chao kamili kuikabili Azam wakiwa na tahadhari kubwa dhidi yao huku akikanusha ripoti zinazoarifu kwamba Simba na Yanga huwa zinawajali nyota wake kimaslahi pindi ifikapo siku ya mechi kubwa

Kamati ya mashindano hayo imewahakikishia usalama mashabiki wa soka wanaotarajia kujitokeza kushuhudia mtanange huo ambapo katibu  wake Said Hamis ameiambia Kipenga ya EA Radio kwamba tayari wameshafanyia marekebisho baadhi ya dosari zilizojitokeza kunako mchezo wa nusu fainali uliozikutanisha Simba na Yanga ambao baadhi ya mashabiki waliokuwa na tiketi walishindwa kuingia uwanjani

 

 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa