Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Nani kuizuia Brooklyn Nets ya Kevin Durrant NBA?

Jumanne , 8th Jun , 2021

Timu ya Brooklyn Nets imeibuka na ushindi wa alama 125 kwa 86 dhidi ya Milwaukee Bucks kwenye mchezo wa mzunguko wa pili wa nusu fainali ya ligi ya kikapu nchini Marekani kwa ukanda wa Mashariki kwenye mchezo uliochezwa usiku wa kuamkia leo.

Kevin Durrant wa Brooklyn Nets akirusha mpira nje ya eneo la D na kufanikiwa kuupita kwenye kikapu na kupata alama tatu '3-Point made' mbele ya Giannis Antetokounpo wa Milwaukee Bucks.

Nets imeibuka na ushindi huo mnono baada ya nyota wake tegemezi Kevin Durrant kuonesha kiwango bora na kuwa nyota wa mchezo kwa kufikisha alama 32 nyingi kwenye mchezo huo kuliko mchezaaji yeyote, rebaundi 4 na assisti 6 na kuibeba Nets kwa mara nyingine tena.

Bila hata ya uwepo wa mlinzi wake tegemezi James Harden anayesumbuliwa na maumivu ya misuli lakini Kyrie Irving hakuwa mnyonge kwani alififkisha alama 22, rebaundi 5 na assisti 6 na hata Blake Griffin aliyeanza mchezo huo alionesha kiwango bora na kushangaza wengi.

Griffin alikuwa mwiba mkali kwa Bucks licha ya kucheza dk25' pekee lakini alifanikiwa kupata alama 7, rebaundi 8 na assisti 1 ilhali upande wa Bucks, Giannis Antetokounpo alishindwa kuonesha cheche kali zaidi mbele ya Durrant kwani alipata alama 18, rebaundi 11 na assisti 4.

Katika kujikusanyia alama hizo, Durrant alirusha mpira mara 6 kujaribu kufunga nje ya eneo la D '3-Point made' na kufanikiwa kufunga mara 4 jambo lililomfanya aweke rekodi ya kushika nafasi ya saba kwa wachezaji wenye '3-Point made' nyingi zaidi 321 kwenye historia ya NBA ya muda wote.

Durrant anamfukuzia nyota mwenzake wa Nets, James Harden mwenye 336 na kushika nafasi ya tano, Lebron James wa Los Angeles Lakers mwenye 432 na kushika nafasi ya pili huku kinara wa mitupo hiyo ni Stephen Curry wa Golden State Warriors mwenye '3-point made' 470.

Ushindi huo ni wa pili mfululizo kwa Brooklyn Nets ambao wanazidi kuendeleza moto wao kwenye michezo hiyo ya NBA Playoff na hata wengine kuwatabiria ubingwa, Bucks wanamlima wa kupindua matokeo kwani wanahitaji kuwasimamisha Nets kabla ya hawajaondoshwa.

Michezo ya mtoano ya NBA itakayoendelea leo kwenye mzunguko wa kwanza kwenye nusu fainali kwa ukanda wa Mashariki ni Philadelphia 76ers watakaokipiga na Atalanta Hawks saa nane na nusu usiku huku Utah Jazz watacheza na Los Angeles Clippers saa 11:00 Alfajiri ya kuamkia kesho.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa