Enock Atta Agyei
Klabu ya Azam FC imethibitisha kupokea taarifa kutoka chama cha soka nchini Ghana, juu ya kuitwa kwa Atta kwenye timu ya taifa ya Ghana ya umri chini ya miaka 20 inayokabiliwa na michuano ya AFCON U20.
''Hongera Enock Atta, kwa kuitwa timu ya Taifa ya Ghana chini ya umri wa miaka 20, 'Black Satellite' kwa ajili ya Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON U-20) zitakazofanyika nchini Niger kuanzia Februari 2 hadi 17 mwaka huu'', imeeleza taarifa ya Azam FC.
Mara nyingi makocha wengi wa mataifa ya Magharibi wamekuwa wakitazama zaidi wachezaji wanaocheza Ulaya lakini uwezo wa kinda huyo aliyesajiliwa Azam FC mwaka 2016 umewashawishi kumjumuisha katika kikosi hicho.
