
Mmoja wa waandaaji ambaye pia ni kocha wa tenisi Salum Mvita amesema kuwa hivi sasa wapo katika harakati za kuhakikisha mashindano hayo yanafanyika kama ilivyopangwa.
Mvita amesema, kikubwa wanachotafuta ni fedha ili kuhakikisha wanafanikisha kila walichopanga ambapo wanahitaji kuhakikisha mpaka Desemba mwaka huu wawe wameshaandaa mashindano yasiyopungua matano.