Haji Manara
Kupitia ukurasa wake wa Instagrma, Haji Manara amewapa pole mashabiki wa klabu hiyo na kuwapa ahadi kuwa Simba lazima ipate pointi 6 za nyumbani na itafuzu hatua inayofuata ya michuano hiyo.
Simba imepoteza mchezo wa pili mfululizo wa ugenini, kwa idadi sawa ya mabao 5-0. Mchezo wa kwanza ukiwa dhidi ya AS Vita Club ya DR Congo.
Wekundu hao wa Msimbazi bado wako katika nafasi ya tatu kwa pointi tatu, wanayo nafasi ya kusonga mbele endapo watafanikiwa kushinda michezo yao yote iliyobakia, miwili wakicheza uwanja wao wa nyumbani na mchezo mmoja wakicheza ugenini dhidi ya JS Saoura.







