
Mashabiki wa Simba
Simba kupitia kwa msemaji wake Haji Manara imesema kiingilio cha chini ni shilingi 5,000 huku cha juu kikiwa ni laki moja.
''Viingilio vya mchezo mzunguko ni 5,000 huku VIP B ikiwa ni 10,000 lakini tutakuwa na tiketi za Platinums ambayo ni 100,000 itajumuisha kuchukuliwa na 'Luxury bus' kutoka Serena Hotel na kusindikizwa na polisi, jezi mpya ya Simba, 'Bites na soft drinks' muda wote utakaokuwa uwanjani pamoja na kurejeshwa Serena'', - Manara.
''Tunawasihi sana wanasimba na washabiki wote tujae kama kawaida yetu Jumamosi, na tuje kuhanikiza, tuje tukijua ujaji wetu ndio silaha yetu'', ameongeza Manara.