Jesse Lingard
Lingard anashinda tuzo hii baada ya kuikosa miezi mwili iliyopita mwezi Februari na Machi ambapo alishindwa kuitwaa tuzo hiyo. Hii ilikuwa ni mara ya tatu mfululizo Lingard anaingia kwenye kinyanganyiro cha kuwania tuzo ya mchezaji bora wa mwezi.
Winga huyu yupo West Ham kwa mkopo akitokea Manchester United, na ametwaa tuzo hii baada ya kuwashinda wachezaji Trent Alexander Arnold, Stuart Dallas, Mason Greenwood, Kelech Ihenacho, Matheus Pereira, Allan Saint Maximini na Chris Wood,alioingia nao fainali.
Steve Bruce
Na kocha Steve Bruce wa Newcatle United ameshinda tuzo ya kocha bora wa mwezi huo ikiwa ni kwa mara ya kwanza anashinda tuzo hiyo katika kipindi cha miaka 19. Bruce aliiongoza Newcastle kushinda michezo mwili na kutoka sare michezo miwili ndani ya mwezi Aprili kwenye michezo minne.
Steve Bruce ametwaa tuzo hiyo akiwashinda makocha Sam Allardyce, Marcelo Bielsa na Ole Gunnar Solskjaer