Laighton Baines akishangilia moja ya mabao aliyoyafunga akiichezea Everton
Akiwa amedumu kwa miaka 13 katika timu ya Everton ambayo ilimsajili kutoka timu ya Wigan Athletics mwaka 2007
Baines ambaye ni raia wa Uingereza amestaafu rasmi katika mchezo wa mwisho wa msimu uliyochezwa jumapili hii dhidi ya AFC Bournemouth akiwa na umri wa miaka 35 ,ambapo aliichezea timu hiyo michezo 420 na kuifungia magoli 39 Licha ya kuwa ni mlinzi alikuwa na uwezo mkubwa wa kufunga magoli.
Mchezaji huyu alikuwa moja ya wachezaji wa Everton waliyewahi kuja nchini Tanzania na kucheza mchezo dhid ya Gor Mahia akiwa na nyota wengine kadhaa kama Wayne Rooney, Yanick Bolasie, Morgan Schneiderling ,Aaron Lennon, Michael Keane na wengineo.
Mnamo mwaka 2013, Klabu ya Manchester United iliwania saini yake kufuatia mapendekezo ya aliyekua kocha wao wa zamani David Moyes ingawa mpango huo haukufanikiwa.








