Jumatatu , 27th Jul , 2020

Leighton Baines ni mchezaji mkongwe wa Everton ambaye amestaafu rasmi mchezo wa soka baada ya kuutumikia kwa miaka 18 katika vilabu viwili tofauti vya ligi kuu ya England ambavyo ni Everton na Wigan Athletics.

Laighton Baines akishangilia moja ya mabao aliyoyafunga akiichezea Everton

Akiwa amedumu kwa miaka  13 katika timu ya Everton ambayo ilimsajili kutoka  timu ya Wigan  Athletics mwaka 2007

Baines ambaye ni raia wa Uingereza amestaafu rasmi katika mchezo wa mwisho wa msimu uliyochezwa jumapili hii dhidi ya  AFC Bournemouth akiwa na umri wa miaka 35 ,ambapo aliichezea timu hiyo michezo 420 na kuifungia magoli 39   Licha ya kuwa ni mlinzi alikuwa na uwezo mkubwa wa kufunga magoli.

Mchezaji huyu alikuwa moja ya wachezaji wa Everton waliyewahi kuja nchini  Tanzania na kucheza mchezo dhid ya Gor Mahia akiwa na nyota wengine kadhaa kama Wayne Rooney, Yanick Bolasie, Morgan Schneiderling ,Aaron Lennon, Michael Keane na wengineo.

Mnamo mwaka 2013, Klabu ya Manchester United iliwania saini yake kufuatia mapendekezo ya aliyekua kocha wao wa zamani David Moyes ingawa mpango huo haukufanikiwa.