
Emmanuel Shija kabla ya kupanda ulingoni huko India,Muay Thai Style Club
Emmanuel Shija ambaye ameshiriki mashindano mbali mbali duniani amesema ameweza kufanikiwa kimataifa kutokana na mafunzo aliyoyapitia katika nchi mbalimbali duniani ambako alitunukiwa vyeti baada ya kuhitimu.
Shija amesema amezunguka mabara yote duniani akicheza mchezo huo na mwaka 2012 alishiriki Tamasha la Amani na Michezo mjini Tehran lililoandaliwa na serikali ya Irani chini ya Rais mstaafu wa nchi hiyo mheshimiwa Mahmoud Ahmadinejad.