Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Coastal wakanusha, kumfuta kazi kocha Mgunda

Jumatatu , 3rd Mei , 2021

Klabu ya Coastal Union ya Tanga kupitia kwa katibu mkuu wake Rashid Mgweno, imekanusha taarifa za kumfuta kazi kocha mkuu wa kikosi hicho Juma Mgunda na imesisitiza kuwa bado wanamipango ya muda mrefu na kocha huyo.

Kocha Juma Mgunda (katika waliosimama) akiwa na wachezaji wa Coastal Union

Katibu huyo wa Coastal Rashid Mgweno ametolea ufafanuzi taarifa za kocha Mgunda kufutwa kazi na amesema

“Hizi taarifa si za kweli na hazina ukweli hata kidogo kwa sababu ni mwalimu ambaye bado tuponaye kwenye mipango ya muda mrefu ya timu. Kwa hiyo ukinambia kwamba zimetoka taarifa tumeacha sisi wenyewe zilitushitua na ilituchanganya kwa sababu hatukujua chanzo chake kilikuwa ni nini na walikuwa na lengo gani kwenye kuzusha hizo taarifa.”

“Naomba nizikanushe hizi taarifa, na niseme Mwalimu Juma bado tupo naye na tunamkataba naye na tuna mipango naye endelevu ambayo tunaamini kabisa yeye atatufikisha ambako tunataka kufika.”

Mapema leo asubuhi zilitoka taarifa ambazo zilidai kuwa klabu hiyo ya Tanga imeachana na kocha mgunda kutokana na mwenendo mbaya wa matokeo wa kikosi hicho kufuatia kuondolewa kwenye michuano ya kombe la shirikiso ya Azam Sports Federation Cup na Mwadui FC kwa kufungwa kwa mabao 2-0 katika hatua ya 16 bora.

Kwenye msimamo wa Ligi Kuu wagosi wakaya wapo nafasi ya 10 wakiwa na alama 33, ikiwa ni tofauti ya alama tano kutoka kwenye mstari wa kushuka daraja. Katika michezo 10 ya mwisho ya Ligi Kuu Coastal imeshinda michezo minne, imetoka sare kwenye mchezo mmoja na wamefungwa michezo mitano.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa