Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Chirwa aachwa safari ya Yanga

Jumamosi , 17th Feb , 2018

Klabu ya soka ya Yanga ambayo inaiwakilisha Tanzania kwenye michuano ya ligi ya mabingwa Afrika inatarajia kuondoka nchini kesho kwenda Shelisheli huku nyota wake Obrey Chirwa akiachwa nje ya kikosi.

Akiongea na waandishi wa habari leo afisa habari wa Yanga Dismas Ten amesema maandalizi ya safari hiyo yamekamilika na timu itasafiri na nyota 20 lakini Chirwa atakosekana.

''Yanga SC inatarajia kusafiri kesho asubuhi kueleka Shelisheli tayari kwa mchezo wa marejeano na wenyeji  St. Louis FC kwenye ligi ya mabingwa Afrika mchezo uliopangwa kuchezwa jumatano ijayo Stade Liete'', amesema.

Ten ameongeza kuwa jumla ya nyota 20 na viongozi 10 kati yao 8 kutoka benchi la ufundi watasafiri lakini mshambuliaji Obrey Chirwa hatakuwepo kwenye kikosi hicho kwasababu ya maumivu ya misuli aliyopata kwenye mchezo dhidi ya Majiamaji.

Pia kiungo Thabani Kamusoko ambaye amepona majeraha yake hivi karibuni na kuanza mazoezi mepesi pia ameondolewa kwenye orodha ya nyota ambao wangesafiri kuelekea Shelisheli ili apate muda wa kujifua zaidi kurejesha makali yake.
 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa