
Michuano hiyo itazinduliwa rasmi hapo kesho kwa kuchezwa mchezo wa kundi B kati ya Burundi na Zanzibar Heroes kutoka visiwani Zanzibar ikifuatiwa na mchezo wa kundi A kati ya mwenyeji wa michuano hiyo Ethiopia dhidi ya Rwanda.
Michuano hiyo inatarajiwa kuendelea kutimua vumbi hapo Jumapili ambapo timu za kundi A The Kilimanjaro Stars ya Tanzania itamenyana na Somalia huku ukifuatiwa na mchezo wa kundi B kati ya Kenya na Uganda.