Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Burundi kutumia dimba la Mkapa kufuzu AFCON

Alhamisi , 12th Mei , 2022

Timu ya taifa ya Burundi 'The Swallows' watakuwa wenyeji wa Cameroon katika mchezo wa Kundi C wa kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2023 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, Tanzania.

(Uwanja wa Benjamin Mkapa - jijini Dar es Salaam)

Alexandre Muyenge, Rais wa Shirikisho la Soka la Burundi alithibitisha kwa Cecafa kwamba watatumia Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dare es salaam kama uwanja wao wa nyumbani.

“Kwa kuwa hakuna Uwanja wetu hata mmoja ulioidhinishwa na CAF, tumeamua kuutumia Uwanja wa Tanzania kama uwanja wa nyumbani kwa mechi zetu za kufuzu AFCON 2023,” alisema Muyenge.

Baada ya kucheza mchezo wao wa kwanza wa Kundi C kwa kuwafuata Namibia nyumbani kwao, baadae tarehe 4 mwezi Juni The Swallows watakuwa wenyeji wa Indomitable Lions ya Cameroon siku nne baadaye jijini Dar es Salaam.Wanachama wengine wa CECAFA ambao hawatatumia Viwanja vyao vya nyumbani kwa sababu havijaruhusiwa na CAF ni pamoja na Sudan Kusini na Ethiopia.

Sudan Kusini itatumia Uwanja wa St. Marys Kitende wa nchini Uganda kuwa uwanja wao wa nyumbani, huku Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka la Ethiopia (EFF), Bahiru Tilahun Limenih akisema watacheza michezo yao ya nyumbani kati ya nchi za Malawi au Afrika Kusini.

Shirikisho la Soka la Rwanda (FERWAFA) pia linasubiri kuidhinishiwa Uwanja na CAF. Timu za CECAFA zitakazochuana kuwania kufuzu AFCON 2023 ni pamoja na Sudan, Ethiopia, Uganda, Rwanda, Burundi, Sudan Kusini, Kenya na Tanzania.

 

HABARI ZAIDI

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji