Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Biashara United mzigoni leo kombe la Shirkisho CAF

Ijumaa , 10th Sep , 2021

Klabu ya Biashara United Mara kutoka mkoani Mara inataraji kushuka dimbani saa 12:00 Jioni ya leo Septemba 10, 2021 ugenini dhidi ya Dikhil ya nchini Djibout kwenye uwanja wa 'Stade De Vulle' kwenye mchezo wa hatua ya awali ya mtoano kuwania kufuzu makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Kikosi cha Azam kikiendelea na Mazoezi (juu kushoto), Yanga nao wakiwa mazoezini (chini kushoto) na kikosi cha Biashara United Mara kabla ya kucheza moja ya mchezo wake wa kirafiki.

Biashara United Mara ambayo inataraji kucheza michezo ya michuano hiyo kwa mara ya kwanza tokea kuanzishwa kwa klabu hiyo miaka 8 iliyopita, iliondoka mchini usiku wa kuamkia leo kuelekea nchini Djibout kwa kupitia nchini Ethiopia baada ya jana kukwama uwanja wa ndege wa kimataifa wa JK Nyerere kwa sababu baadhi ya wachezaji wake kutokamilisha taarifa za kusafiria.

Kwa upande mwingine, Klabu ya Azam imethibitisha kukamilisha maandalizi ya mchezo wake dhidi ya Horseed ya Somalia wa hatua ya awali ya mtoano kuwania kufuzu makundi ya Kombe la Shirikisho barani Afrika mchezo utakaochezwa kwenye dimba la Chamazi jijini Dar es Salaam saa 1:00 usiku wa   kesho Jumamosi ya Septemba 11, 2021.

Azam itacheza mchezo huo bila ya mfungaji wa klabu hiyo wa msimu uliopita, Prince Dube ambaye jana Septemba 9, 2021 amefanyiwa upasuaji salama katika hospitali ya Vicent Pelloti jijini Cape Town, Afrika Kusini na sasa hali yake ni nzuri na Jumatatu Septemba 13 atarejea nchini.

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu ya Azam, Zacharia Thabiti amesema Dube alikuwa anapata maumivu makali kwenye maeneo la chini ya kitovu kushoto pindi akaijaribu kukimbia kwa kasi hivyo wanaimani tatizo hilo litapona na Dube kurejea kwenye utimamu wake wa kawaida.

Kwa upande wa mwakilishi mwingine wa Tanzania kwenye michezo ya kuwania kufuzu hatua ya makundi ya michuano ya klabu bingwa Afrika ni Yanga ambao wanaratiba ya kukipiga dhidi ya Rivers United ya Nigeria saa 11:00 jioni kwenye dimba la BW Mkapa kukiwa na tamko la CAF kuzuia watazamaji kuingia uwanjani kushuhudia mchezo huo kutokana na uwepo wa Covid-19.

Kuelekea kwenye mchezo huo, Msemaji wa Yanga, Haji Manara amethibitisha leo Septemba 10, 2021 kuwa bado hawajapokea barua ya majibu kutoka CAF juu ya hati za usajili wa kimataifa kwa wachezaji wao Djuma Shabani, Fiston Mayele na Khalid Aucho hivyo hawatokupewo kwenye mchezo huo siku ya Jumapili hii.

Manara alishawatoa shaka wanayanga kwa kusema, Yanga ni timu kubwa hivyo imesajili wachezaji wengi pamoja na waliopo hivyo wanauwezo wa kucheza na Rivers United bila ya uwepo wa nyota hao watatu licha ya kukiri watatu hao ni wachezaji wenye uwezo mkubwa sana kuisaidia Yanga kimataifa.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa