Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Azam yaendeleza moto VPL

Jumamosi , 26th Sep , 2020

Matajiri wa Chamazi, Azam Football Club hii leo wametoa kichapo cha bao moja kwa sifuri kwa timu ya Tanzania Prison kwenye mchezo wa raundi ya nne ya Ligi kuu Vodacom Tanzania Bara uliopigwa katika uwanja wa Nelson Mandela Mkoani Rukwa.

Mshambuliaji wa Azam FC Prince Dube amefikisha mabao 3 ya ligi kuu Tanzania bara VPL

Bao pekee la Azam limefungwa na nyota wao raia wa Zimbabwe Prince Dube mnamo dakika ya 89.

Mchezo ulikuwa wa ushindani wa aina yake kwani timu zote zilikuwa zikishambuliana sana, ila shukrani ziende kwa magoli kipa wa pande zote kwasababu waliweza kuokoa michomo mingi.

Kwa matokeo haya sasa Azam inafikisha alama kumi na mbili na inaongoza katika msimamo wa ligi na haijapoteza mchezo hata mmoja imeshinda michezo yote minne. Prison yenyewe inasalia katika nafasi ya kumi na moja na alama zake nne.

Na mshambuliaji wa Azam FC Prince Dube amefikisha mabao matatu lakini pia goli kipa David Kisu hajaruhusu bao hata moja katika michezo yote minne.

Mchezo wa mapema uliochezwa majira ya saa nane mchana katika uwanja wa Ushirika Moshi na wenyeji Polisi Tanzania wameibuka na ushindi wa mabao matatu kwa sifuri dhidi ya Dodoma Jiji.

Mabao ya Polisi yalifungwa na Mshambuliaji wao hatari Marcel Kaheza dakika ya 11 na 61 huku lingine likifungwa Tariq Seif kiakala dakika ya 39.

Huu ni mchezo wa kwanza kwa Dodoma Jiji FC kufungwa kwani kabla ya leo walishinda mechi mbili na kupata sare moja ikiwa na alama zake saba wakiwa bafasi ya sita, wakati Polisi wanashinda mchezo wao wa pili msimu huu na wanafikisha alama saba pia wakiwa nafasi ya nne kwenye msimamo.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea