Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Azam FC yazichimba mkwara Simba na Yanga

Jumanne , 13th Feb , 2018

Baada ya kutofanya vizuri kwenye mechi mbili zilizopita, Kocha Msaidizi wa Azam FC, Idd Cheche, ameweka wazi kuwa huo si mwisho wa timu hiyo kwenye vita ya kuwania ubingwa wa Ligi Kuu kwani hata vinara Simba na Yanga wanaweza kufungwa.

Katika mechi nne zilizopita za ligi Azam FC imefanikiwa kuibuka na ushindi kwenye mchezo mmoja dhidi ya Ndanda (3-1), ikipoteza dhidi ya Yanga (2-1) na Simba (1-0) kabla ya jana kutoka sare ugenini na Kagera Sugar (1-1).

“Sisi tunasema bado tunamechi nyingi kwa sababu kupoteza mechi moja au mbili sio kukosa ubingwa ni kama vile mtu kuumwa ambapo kuumwa sio kufa, unaumwa unajiangalia nini tatizo unalifanyia kazi unajaribu kupambana upone na Yanga na Simba nao wanaweza kupoteza'', amesema kkocha msaidizi Idd Cheche.

Matokeo hayo kiujumla yameifanya Azam FC kufikisha pointi 34 ikiwa nafasi ya tatu kwenye msimamo sawa na Yanga iliyonafasi ya pili kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa huku Simba ikiwa kileleni kwa pointi 41, zote mbili zikiwa na mchezo mmoja mkononi.

Kikosi cha Azam FC kinatarajia kuanza safari kuelekea mkoani Iringa,kesho Jumatano alfajiri kwaajili ya kucheza na Lipuli kwenye mchezo wa raundi ya 19 Ijumaa jioni.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa