Ijumaa , 19th Jul , 2019

Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar Es Salaam, Camilius Wambura, amethibitisha kumuita msanii wa filamu nchini,  Irene Uwoya na Steve Nyerere, kufuatia kitendo alichokifanya cha kuwarushia pesa, wanahabari katika  mkutano uliofanyika mapema mwa wiki hii.

Irene Uwoya

Kamanda Wambura amesema, walimuita na kumhoji siku ya Julai 17, ambapo alidhaminiwa na kutoka kwa dhamana huku Jeshi la Polisi likiendelea na uchunguzi.

''Waliitwa kuja, walionekana kwenye clip moja, Yule Irene alionekana anatupa fedha, kwa wanahabrari, na alihojiwa na kudhaminiwa na uchunguzi mwingine unaendelea'' amesema Kamanda Wambura.

Ikumbukwe kuwa  siku ya Julai 15, Irene Uwoya, alionekana katika baadhi ya video zilizosambaa mitandaoni, akirusha fedha kwa wanahabari, kitendo kilichotafsiriwa kuwa ni udhalilishaji na Irene alikiri kukosea na kuomba radhi kupitia ukurasa wake wa Instagram.