Jumanne , 6th Dec , 2022

Bunge la nchini Indonesia limepitisha sheria mpya inayokataza watu kujamiana kama hawajafunga ndoa, ikijumuisha mpaka wageni wanaoingia nchini humo.

Kupitia sheria hiyo mpya wapenzi ambao watashiriki tendo la ndoa na hawajafunga ndoa watafungwa jela mwaka mmoja kwa kuvunja sheria.

Pia ni marufuku kwa mwanamke na mwanaume kuishi pamoja bila ndoa, kifungo chake ni miezi 6 ukivunja sheria.