
Mfanyabiashara Elon Musk.
Kulingana na mtandao wa Bloomberg, Musk (51) ameona utajiri wake ukishuka hadi dola bilioni 137 baada ya hisa za Tesla kushuka katika wiki za hivi karibuni ikiwamo kushuka kwa hisa 11% Jumanne ya wiki iliyopita.
Elon Musk alibakia kuwa mtu tajiri zaidi ulimwenguni kwa utajiri uliofikia dola bilioni 340 mnamo Novemba 4, 2021 mpaka alipopinduliwa na tajiri wa Ufaransa Bernard Arnault mwezi Disemba.