Jumatatu , 30th Mei , 2022

Mchezaji wa zamani wa Rangers na Manchester United, Andy Goram amebakisha miezi 6 ya kuendelea kuishi duniani baada ya kugundulika ana ugonjwa wa saratani.

Andy aliwahi kucheza Manchester United kwa mkopo mwaka 2000.

Andy (58) alianza kuumwa mwezi mmoja uliopita na alipoanza kuumwa alichukulia hali ya kawaida tu ,hali ilivyoanza kubadilika aliwasiliana na daktari wake na kupelekwa hospitali.

Baada ya vipimo majibu yakaja ana ugonjwa wa saratani ambao umesambaa kwenye ini, na mapafu na ataweza kuishi kwa miezi 6 akiwa na ugonjwa huo.