Jumatatu , 11th Dec , 2023

Wasanii wa BongoFleva nchini Tanzania Alikiba, Lady Jaydee, Chege na Temba, Weusi wamejitolea kuchangia fedha katika taasisi ya mkongwe wa HipHop Professor Jay 'Professor Jay Foundation' ya kusaidia wagonjwa wa figo nchini.

Picha ya msanii Professor Jay

Taasisi hiyo imezinduliwa rasmi siku ya jana Mlimani City Dar es Salaam ikihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, CHADEMA, wasanii wa filamu na muziki pamoja na waandishi wa habari.