Jumatano , 9th Nov , 2016

Leo tarehe 9 Novemba 2016 Marekani imeandika historia kwa kumchagua Donald Trump kuwa Rais wa taifa hilo, mtu ambaye alikuwa 'talk of the world' kwa mtazamo wake juu ya watu weusi.

Donald Trump - Rais Mteule wa Marekani

 

Baada ya ushindi huo ulioshangaza dunia watu mbalimbali wamefunguka hisia zao ikiwemo wasanii mbalimbali wa ndani na nje ya bongo na kuandika yale ya moyoni kuhusu ushindi wa Donald Trump.

Afande Sele ...."Chizi kalogwa tena....Don Trump Ile Kweli imemuweka Huru...Siasa za unoknok na Nidhamu ya woga na vipotelee mbali kabisa #Sisi".

Dogo Janja ..."Usiyempenda kaja mbwa kala mbwa @realDonaldTrump". 

Mwana FA... 'Kabisa..i mean we are not Americans so ni suala lao lakini yoo,doesnt look good kwetu wote man".

Madee ....Watu wanamaneno /et America inayoweza kuongozwa na mwanamke apa duniani ni American chips tu ya kinondoni

Vugu vugu hilo limeendela mpaka kwa wasanii wa Marekani, ambapo wasanii wengi wenye asili ya Afrika wameonyesha kutofurahishwa na ushindi wa Donald Trump.

Snoop Dog ...... Worst Day in America  9/11, 2nd worst day in Maerica 11/9

Jidenna .....I apologize to the world on behalf of my country #ElectionDay

Lakini pia ushindi huo umeambatana na pongezi mbalimbali zikiwemo za aliyekuwa mpinzani wake Hillary Clinton, na viongozi mbalimbali wa nchi tofauti duniani.