Jumatano , 9th Sep , 2015

Tetesi za star wa muziki wa nchini Uganda, Rema Namakula kuzuiwa kuingia Marekani na kurudishwa kwa nguvu nyumbani na mamlaka ya uhamiaji ya nchi hiyo, zimeendelea kupata nguvu baada ya barua inayoaminika kuwa inatoka kwa mamlaka hiyo kuibuka.

staa wa muziki wa nchini Uganda, Rema Namakula

Barua hiyo inayotoa maelekezo ya kurejeshwa Uganda kwa Rema, ikionyesha kuandikwa tarehe 6 mwezi Septemba kutoka huko Detroit, na kupatikana kwake kukifafanuliwa kuwa ni kutokana ushirikiano na mamlaka ya uhamiaji chini ya sheria ya uhuru wa kupata taarifa.

Barua hiyo inayeyusha utetezi mzima wa Rema hivi karibuni kuwa aliamua kurejea nchini ghafla na kukatisha safari yake kufuatia kupata ujumbe kuwa mwanawe amezidiwa na amelazwa hospitali.