Picha ya msanii wa BongoFleva Dully Sykes
Dully Sykes amesema sasa hivi hana stori na watoto wa kike,ila kwa wakati ule anapata kashfa hizo hata yeye alikuwa ana umri mdogo wa makamo ya kiuwanafunzi kwa hiyo haikuwa shida kuwapata.
"Unajua sio kila anayebaka chanzo anakuwa ni yeye pengine chanzo ni mbakwaji, kwa kipindi kile watu wanasikia napenda wanafunzi hata mimi nilikuwa mwanafunzi pia japo nilikuwa sipo shule, lakini kwa makamo yale yalikuwa ya kiuwanafunzi kwa hiyo kuwapata haikuwa mbaya" amesema Dully Sykes.
Aidha Dully Sykes ameendelea kusema "Nilivyokuwa mtu mzima nikaanza kuchukua watu wazima wenzangu hadi nikapata nao watoto kabisa na sijawahi tena kuchukua videnti" ameongeza.



