Alhamisi , 14th Dec , 2023

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limetoa taarifa ya kuufungia wimbo mpya wa Madee aliouchia Disemba 13 kwa kosa kubwa la kukiuka kanuni za BASATA za mwaka 2018 na mwongozo wa maadili wa kazi za sanaa mwaka 2023.

Madee

Madee amepewa adhabu ya kulipa faini ya Tsh Milioni 3 na kutofanya shughuli zozote za kisanii mpaka atakapolipa faini hiyo pia Producer wa ngoma hiyo Mr T Touch naye anatakiwa kulipa faini ya Tsh Milioni 1.